Nameless na Wahu washerehekea miaka 14 katika ndoa

Hivi leo, wanamziki bomba wa mumu humu kenya, Nameless na Wahu wanasherehekea maadhimisho ya miaka kumi na nne (14), tangu wafunge ndoa.

Kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram, Wahu alitudhihirishia kuwa ndoa yao imekuwa ya kufana na hana lolote linaloweza kumfanya ajute kufunga ndoa za maisha na mpenzi wake Nameless.

Katika mtandao wa Instagram aliandika kuwa, katika ndoa yao, wamecheka, wemelia, wamepigana, wakatafuta pesa, wakapoteza pesa, wakakubaliana na kutokubaliana na mambo mengi na zaidi ya hayo, Wahu akasema kuwa amejua kuwa anaweza kumtegemea mpenzi wake kwa lolote lile.

 Licha ya hayo, Wahu amemshukuru mpenzi wake kwa kumpenda vilivyo pasi na yeye kuwa mtu kamili.

''oooooooowwww!!! Its our 14th wedding anniversary!!! Where did the time go! 😄😄

What can I say babe... We've laughed, cried, faught, made up, made money, lost money, agreed, disagreed and throughout this rollercoaster called life, I've always known I can count on you... my best friend, lover, cheerleader..my ride or die.

Thank you for loving me with all my imperfections.

Happy 14th anniversary . Here's to 100 more!!! 🥂🥂''

Vilevile, pasi na kuwa na maisha matamu ya ndoa, wapenzi hawa wamebarikiwa na watoto wawili, mabinti warembo sana, asiee!vidosho wa kuwakata wanaume shingo.

Ama kwa hakika, Mapenzi ni Matamu !