‘ Napenda mashosho.’ 'Kahaba mwanamume aeleza anavyoishi kama mfalme kwa kuwapa ngono wanawake Nairobi

Mara  kadhaa umeskia kuhusu visa vya   makahaba wanawake  na jinsi wanavyoendesha shughuli zao za kuiuza miili yao .

Lakini sasa fahamu kwamba kuna wanaume ambao pia hufanya ukahaba kwa kuuza miili yao na kulipwa! Sikuamini kuna wanaume wanaofanya kazi kama hiyo hadi pale  Justus  Moto alipokubali kunisimulia  maisha yake kama kahaba wa kiume  na jinsi anavyoishi maisha  ya starehe  kwa hisani ya  wanawake kadhaa ambao ni wateja wake na wanaofahamu jinsi anavyowahudumia kwa kuwapa kila raha wanazotaka katika nyumba zao .

Justus anasema alijipata katika kazi hiyo wakati alipokuwa Model wa kiume na baada ya msururu wa kazi za maonyesho akivalia nguo za  lebo moja ya  Afrika Kusini. Mwanzoni aliwavutia wanawake wa rika lake ambao wengi  walivutiwa na  kuunga kwa mwili wake na mara nyingi uhusiano  kati yake na wasichana hao uliishia kwa One Night  stands  ngono za usiku mmoja bila  makubaliano ya uhusiano wa kudumu. Muda sio mrefu, Justus aligundua kwamba  kuna wenzake katika  kampuni yake ya modeling ambao walikuwa wakiishi maisha ya gharama ya juu, na  alishangaa waliwezaje kugharamia  mtindo wao wa maisha .

Akiendelea kujikuna kichwa kugundua siri, alinong’onezewa  kuhusu  ‘biashara’ ya pembeni iliyokuwa ikinoga kwa Models wa kampuni ile ya  kuwapa huduma za  ngono wanawake  ambao hawakuwa na  waume, na wa umri wa juu na waliokuwa na pesa kama njugu! Justus alijua kwamba  uwanja huo mpya ulioonekana wa kuvutia utamletea matatizo baadaye lakini pia alivutiwa sana na pesa na mtindo wa  maisha ya kifahari ambao ulikuwa umemngoja endapo angekubali kujiingiza katika biashara hiyo. Muda sio mrefu, Justus alikuwa keshafanya uamuzi wake na wateja  walikuwa wengi na walimtaka kila wakati. Mwanzo, mteja alimfahamisha siku ambayo alimhitaji na kupitia kundi la whatsapp, waliunda ratiba. Akina mama hao wengi wao wakiwa wafanyikazi wazito katika mashirika makuu ya umma na kibinafsi na wafanyibiashara  tajika. Biashara hii ya mahakaba wa kiume ipo hapa Kenya na inaendeshwa kwa usiri mkubwa .

‘ Unashangaa kuwaona baadhi ya hata wasanii wakiishi maisha mazuri, kuna kazi inayoendelea chini ya maji na ina pesa’ anafichua  Justus

  Kuhusu malipo, Justus  anasitasita kabla ya kusema kiasi cha fedha ambazo yeye hutoza kwa huduma zake .  Malipo , anasema yanategemewa na muda ambao mteja atataka awe naye. Usiku mzima kwa mfano ni shilingi elfu 25 kwa mteja  ambaye uhudumiwa angalau mara nne kwa mwezi . Wateja wapya hutozwa kiasi cha juu kwa sababu  ya kuweza kuwachuja wale ambao labda wanaleta mchezo katika  ratiba zao na kusalia tu na wateja ambao watakuwa wa kila mara .

 ‘ Kupitia kazi hii ya kisiri ,nimweza kujenga nyumba na hata kuwekeza  hapa Nairobi na mashambani’ Justus anasema .

Justus anasema wengi wa wateja wake ni wanawake wa umri wa juu ambao wametelekezwa na waume zao au ni wajane. Anasema anapenda kuwahudumia wanawake wa umri wa juu kwa sababu hawasumbui na wao hujua wanachotaka pindi tu wanapoagiza kupata huduma zake .

‘ Sisi huwaita mashosho – ni wakarimu and mostly hamsumbuani kuhusu malipo.wanajua nipo kazi na mimi huwasikiza hata wakati ninapoendelea kuwapa starehe zao’ anasema Justus

Justus anasema jamii inafaa kujali maslahi ya wanawake wa umri wa juu kuanzia maiaka 40 ambao hawana wapenzi na wanaohitaji ngono. Anasema  ni ubinafsi kwa watu wa umri wa chini kuwasulubisha wanawake hao ama kufikiria kwamba nao pia hawahitaji joto katika vitanda vyao . Licha ya usiri mkubwa unaohusishwa na biashara yao, Justus anasema ameyaona makubwa na baadhi ya siri za wateja wake  humfanya kububujikwa machozi .

‘ Kuna mteja wangu ambaye mume alimuacha kwa sababu ni  mnene kupindukia, kabla ya kujulishwa kuhusu huduma zangu, alikuwa ameishi miaka mitano bila kushiriki ngono’ anasema  Justus

Justus anaongeza  kusema ;

‘ Wakati mwingine, hata kama wengine watasema ni utani, mimi hujihisi kwamba natekeleza wajibu muhimu kwa jamii, wanawake wanaotumia huduma zangu kupata ngono huridhishwa na kuwezeshwa kuhisi vizuri kama tu watu wengine’ anatamatisha Justus .