‘Nataka mimba!’ Mwanadada asema katika twitter akihofia ‘kufa’ kwa ajili ya Coronavirus

Corona 2
Corona 2
Baada ya  kuthibitishwa kwamba sasa kuna visa vitayu vya virusi vya corona nchini Kenya ,kumekuwa na hofu huku baadhi ya wakenya wakifanya utani kwamba huenda  ni mwisho wa dunia .  Wengi walikimbia sokoni kununua bidhaa za vyakula wakihofu kwamba huenda patatokea uhaba wa vyakula .

Hata hivyo mwanadada mmoja katika twitter ameonekana kuhofishwa  na uwezekano wake kufa kabla hajaitwa mama na hivyo basi ametoa rai kwa  mwanamme aliye tayari kumchukua kama mke ili ampe mimba aweze kujifungua kabla hajafa!

https://twitter.com/JudyLimo5/status/1238691459789922306

Wengi waliomjibu walionekana kufurahishwa na ujumbe wake huo wa ucheshi lakini huwezi kujua labda anaitumia fursa hiyo kuweza kupata mpenzi Kenya sihami!