Ni tabia zipi za ma-deejay unazozichukia?

Deejay (1)
Deejay (1)
Tasnia ya burudani kwa sasa imejaa wanaume na wanawake wengi wanaojituma katika haso za kila siku za kuwapatia watu burudani kwa kutumia sahani za santuri. Kuna ma-deejay wanaofanya kazi kwenye redio, runinga, vilabu na pia kanisani na maeneo mengine ya burudani au tamasha.

Soma hapa:

Hali kadhalika kuna wale wafanyabiashara wamechukua kipaji hiki kama biashara na kufungua shule za kutoa mafunzo kwa vijana wanaotamani kuwa ma-deejay.

Kulikuwepo na dhana kuwa tasnia hii haihitaji masomo shuleni ila kuna baadhi ya ma-deejay kama Creme Dela Creme, Dj Juan, Dj Mo na Sadiq ambao wametokea na kuuzima mtazamo huu.

Pata Uhondo hapa:

Japo huwa tunafurahi sana tunapopata madini mazuri ya miziki inayochezwa na wanasanaa hawa, kuna baadhi ya tabia wanazofanya hazivutii kabisa:

  1. Kufanya mauzo au kujitangaza katikati ya ngoma - Ghafla utakuwa unasikiliza muziki afu deejay ashtukize kwa kutupia pale majina yake kwenye mitandao ya kijamii
  2. Kutuma salamu kwa wapenzi wao na wanadada hususan kwenye vilabu. Utaskia, “Shiro was Githu 44, umesalimiwa” ama “A gyal dem, Beyonce wa Ungwaro niaje?”.
  3. Visauti vya kurembesha ngoma vinachombezwa katikati kama:  ‘you’re chilling with best DJ in Kenya’, ‘come back selecta’,  ‘mbrrrrrcha, awuoooh, thitima’ and ‘your girlfriend’s favourite DJ’.
  4. Deejay kuimba muziki unapocheza- Kazi ya deejay ni kuucheza muziki mashabiki wausikilize ila sio kuimba. Mashabikib wakitaka kuimbiwa wataenda Kosewe au ata kwenye matamasha yanayofanywa na bendi na kutazama na kusikiliza .