‘Nilibeba maiti ya mtoto wangu kwa handbag’ Mwanamke asimulia mateso ya kukosa pesa

Hebu fikiria kuhusu kumpoteza mwanao kisha ukose usaidizi wa kuweza kuisafirisha maiti yake hadi   eneo unalotaka kumzika.Hayo ndio masaibu yaliyomkumba  Ziporah Chiti ambaye aliubeba mwilia wa mtoto wake wa mwaka mmoja kutoka Nairobi hadi Kwale .

Matatizo yake yalianzia  katika hospitali moja hapa Nairobi ambapo mwanawe alikosa kuhudumiwa na madaktari kwa wakati   na kuaga dunia .  kwa sababu alikuwa ametumia pesa nyingi kwa matibabu ya mtoto hakuwa na pesa za kutosha  kutafuta jeneza na kufanikisha usafiri wa mwili wake kutoka jijini hadi Kwale . Chiti alijaribu kutafuta  usaidizi kutoka kwa jamaa na rafiki zake lakini kiasi cha fedha zilizokusanywa hakikutosha kuweza kuusafirisha mwili wa mwanawe .Ni katika hali hiyo alipoamua kwamba liwe liwalo kwani  alipanga kuubeba mwili wa mtoto wake katika mfuko wake wa mkononi kutoka Nairobi hadi kwale .

Aliuchukua mwili  ule hospitalini na kuuweka katika  karatasi na kisha  akaukunja katika  leso na kutumbukiza kwenye begi lake .Hakuna aliyeweza kujua amebeba nini lakini moyoni mwake alihuzunika  sana  kuona kwamba hali ya uchochole ilikuwa ikimlazimu kuusafirisha mwili wa mtoto wake kwa njia ile.

Alifika katika kituo cha mabasi ya kwenda Mombasa mwendo wa saa moja jioni na gari lile  likaondoka .  Akiwa safarini  Chiti alikuwa akibubujikwa machozi abiria wenzake wasijue nini kulikuwa kikimliza na waliotaka kujua zaidi aliwaambia  alikuwa mgonjwa na hivyo basi  maumivu yalikuwa yamemzidi . Begi yake iliyokuwa na mwili wa mtoto wake iliwekwa ndani ya gari katika vyuma vilivyokuwa juu ya kiti chake .Alikumbuka jinsi mlinzi lkwenye mlango wa gari alipomuuliza amebeba nini alimuambia kwamba alikuwa amebeba nguo zake .

‘Nilihofia kwamba iwapo angeamua kuikagua ile begi basi angeupata mwili wa mtoto  wangu,ingekuwa kesi  kwa sababu hakuna angeyeweza kuamini kwamba nimeshindwa kupata pesa za kuusafirisha mwili huo’ anasema Chiti .

Alipofika Mombasa , Chiti hakuwa na muda wa kupumzika na safari ya kwenda Kwale ikaanza .Alichukua gari jingine hadi kwale huku jamaa zake wakimgonja kwa maazishi .Hawakujua kwamba  mwili wa mtoto ulikuwa ukisasafrishwa katika  mkoba wa mkoni na wengi walishangaa walipomuona Chiti akiingia bomani bila jeneza wala msafara wa magari . Alipoingia chumbani aliutoa ule mwili ambao sasa ulikuwa umeathiriwa na joto baada ya safari ndefu iliyoanza siku iliyotangulia .  Baada ya maazishi Chiti hakuweza kupata nguvu za kuja Nairobi kwa sababu wiki mbili zilizopita kabla ya mwanawe kuaga dunia zilikuwa ndefu kwake .Kifo cha mtoto wake kwa sababu ya utepetevu wa madaktari pia kilimpa kumbukumbu ambazo alitaka saba kuzifuta akilini mwake .