Nilimfungisha virago siku ya Valentine,Asema Zari Hassan

11313649_652073814937709_1850145236_n
11313649_652073814937709_1850145236_n
NA NICKSON TOSI

Zari Hassana kando na mishe mishe zake za mahaba na watu wa haiba  ya juu,anafahamika sana namna anavyoishi maisha ya kifahari na kuendesha magari ya haiba ya juu.Kwa muda sasa ,mwadada huyo amekuwa akificha namna alivyoachana na Diamond lakini sasa ameamua kupasua mbarika na kudai kuwa aliwachana na mwanamziki huyo baada ya kuchoshwa na tabia zake za kupenda wanawake.

Kupitia video aliyokuwa ameituma kwenye mtandao wake wa Instagram,Zari alisimulia jinsi alivyomuacha Diamond wakati wapenzi kote ulimwenguni walikuwa wanaadhimisha siku ya wapendanao.

Tazama video yenyewe hapa.

Yanajiri haya sikiu chache tu baada ya Tanasha Donna pia kumkashifu Diamond kwa alisema kuwa anawahadaa wanawake kuingia katika uhusiano na wao na kisha kuwaacha baada ya kuwapa ujauzito .

Tanasha alisimulia jinsi alivyojaribu kuvumilia uhusiano huo wake lakini ikashindikana na kuamua kufunganya.

Vichuna hawa wote wameamua kuishi na pwatoto wao mbali na kutaka kusikia taarifa zozote zinazo wahusisha na Diamond.