'Nilimpa baraka zangu.' Diamond asema Hamisa alimuomba ruhusa kabla ya kuwa video vixen katika wimbo wa Alikiba

Baada ya Alikiba kutoa wimbo wake wa 'dodo' na baby mama wa Diamond Hamisa Mobetto, wengi walibaki midomo wazi huku wakidai kuwa Hamisa alimcheza Diamond.

Wimbo huo ulitolewa tarehe 8, Aprili mwaka huu, baada ya muda Diamond akiwa katika mahojiano alisema kuwa Hamisa alimuomba ruhusa ili ashiriki katika wimbo huo.

Aliongeza na kusema kuwa alimpa baraka zake na kumpa ruhusa na kusema kuwa Alikiba ana haki ya kutoa wimbo na mwanamke atakayependa.

Cha mno alizungumza na kusema pia Baby mamas wake pia nao wana uwezo na fursa ya kuwa katika nyimbo za wasanii.

"Ali has every right to use anyone he pleases in his music videos, my fellow parent also has the right to appear in any video she likes," Diamond said. "Even before shooting the video, she told me Ali Kiba wanted her to appear and was telling me so that I don't watch it later and think otherwise as it came out." Alizungumza Diamond.

Katika wimbo huo, Hamisa alikuwa amevalia mavazi ya malkia na msanii Alikiba alikuwa amevalia mavazi ya mfalme, ni wimbo ambao  uliwaacha wengi wakizungumza wengi.

Baada ya kibao hicho, wawili hao walionekana wakiwa pamoja wakisakata wimbo kama wapenzi wawili.