Nilisingiziwa kuwa nimeuza mfuko wangu wa uzazi - Kansiime

kansiime
kansiime
Msanii mashuhuri kutoka Uganda, Anne Kansiime amezungumzia kuhusu cheche za matusi na maneno machungu ashawahi patana nayo katika mitandao ya kijamii.

Akizungumza katika kipindi cha Bustani la Massawe, Kansiime alifichua kuwa miaka kadhaa iliyopita shabiki mmoja aliwahi msingizia kuwa ameuza mfuko wake wa uzazi (Uterus)

Kulingana na shabiki huyo, Kansiime aliuza mfuko wa uzazi ili ajinufaishe kimaisha na pia ili apate umaarufu.

Madai hayo ni kufuatia shida ya Kansiime ya kutoweza kupata watoto.

Miaka miwili au mitatu iliyopita, walisema kuwa nimeuza mfuko wangu wa uzazi kwa sababu sikuwa napata watoto na mpenzi wangu wa kale.

Pia mimi nilitaka kujua soko la mifuko ya uzazi ili pia niwaelekeze wale ambao wangetaka kununua au kuuza zao. Maneno hayo yalinikera zaidi na yakaniwacha na uchungu mwingi. Alisema Kansiime.

Kansiime alikuwa amefunga ndoa ya kitamaduni na aliyekuwa mpenziwe, Gerald Ojok kwa takriban miaka mitano kabla ya wawili hao kutengana.

Alipoulizwa sababu alidai kuwa anahisi labda alikimbilia ndoa na pia anahisi kuwa yeye ni mgumu kuelewa kwani anajipenda zaidi kuliko anavyompenda yeyote.

Alikiri kuwa mumewe ndiye aliyetoka kwa ndoa na ingawa analipwa fedha nyingi kumliko, haelewi sababu zake kumtenga. Hata hivyo sahii ana mchumba mwingine kwa jina Tukahirwa Abraham almaarufu, Skylanta.

Nahisi labda nilikimbilia ndoa kwani nilitaka kwanza kusoma, nipate kazi kisha nitafute bwana. Ndio nilisoma nikahitimu, nikapata kazi kisha nikapata mwanaume lakini nadhani nilikimbilia ndoa.

Aliongeza,

Hakukuwa na shida ya uaminifu kwa ndoa yetu, ni ukweli nilikuwa na hela kumliko mume wangu lakini hadi wa leo siju mbona aliniwacha.

Mimi ni mtu mgumu kuelewa na mara nyingi nahurumia wanaume ambao hunipenda. Mimi na Sky tutapendana hadi siku tutajua kama tutaishi pamoja.