Maseneta wawili wateule - Beatrice Kwamboka na Mary Seneta walipigana makonde bungeni wakati wa uchaguzi wa naibu mwenyekiti wa kamati ya bunge kuhusu afya .
Patashika ilizuka muda mfupi baada ya seneta wa Narok Ledama Ole Kina kutangazwa mshindi wa kinyang’anyiro hicho dhidi ya Seneta.
Seneta alikuwa akiungwa mkono nan a baadhi ya wanakamati hiyo wakiongozwa na naibu kiranja wa walio wengi Farhiya Ali.
Kulingana na maseneta waliokuwa katika mkutano huo kundi la Farhiya lilitumia sahihi bandia ya seneta Millicent Omanga ili kumpa ushindi Seneta .