https://www.instagram.com/p/CCL3S8Uhom9/
Nderu alizua mhemko mtandaoni baada ya kurushiwa cheche za shutuma na watu wengi kwa kuwaleta wapenzi wa jinsia moja katika kipindi hicho ambapo walionekana wakipika na kufanya densi densi mtandaoni . baadaye watu wengi walianza kumtumia jumbe za kumkashifu kwa upotofu wa maadili wakimtaka aiondoe video hiyo mtandaoni lakini hajatikisika .
Alipoulizwa na Massawe iwapo naye pia ni shoga amesema hilo ni jambo la kibinafsi na atajitokeza endapo itahitajika au wakati ufaao ingawaje kwa sasa amebainisha wazi kwamba anaunga mkono wa jamii ya LGBTQ.
https://www.instagram.com/p/CCIEZkBh7RG/?utm_source=ig_embed
Ameongeza kwamba hatosita kuwaleta tena watu wa jinsia moja katika makala yajayo ya kipindi chake instagram kwani kila mtu anafaa kuheshimu maoni ya wengine .
‘Nakataa kuomba msamaha kwa kuwaruhusu rafiki zangu kuwa jinsi walivyo,nakataa kuomba msamaha kwa kupeperuha episode hiyo kwa sababu ni yangu ,ingawaje naheshimu uamuzi wa wale ambao hawajapendezwa na kipindi hicho’