No Targets:Mageuzi katika Senate hayalengi jamii yoyote asema Munya

Munya
Munya
Waziri wa kilimo  Peter Munya amewakemea viongozi wanaomuunga mkono DP Ruto  wanaodai kwamba mageuzi katika senate yanalenga  jamii Fulani . Amesema mageuzi hayo  katika chama cha Jubilee  yanalenga kukiboresha chama hicho na usimamizi wa serikali bali hakuna jamii inayolengwa .

Munya amesema Ruto amekuwa kikwazo   kwa ajenda ya serikali kwani amekuwa akiwachochea maseneta na wabunge  kusababisha vurugu serikalini na kufanya kuwa vigumu wa rais Uhuru Kenyatta kutekeleza majukumu yake ya utawala . Mirengo miwili ya kisiasa imeibuka ndani ya chama tawala cha Jubilee kati ya wanaomuunga mkono rais Kenyatta na walio katika upande wa naibu wake William  Ruto na kuunda makundi ya  Tangatanga  na  Kieleweke.

Akizungumza katika mkutano na wakulima wa kahawa huko Meru siku ya jumamosi Munya amesema  rais Kenyatta hajakiuka sheria au katiba kwani anatumia maamlaka yake kufanikisha demokrasia .Munya  amesema kuondolewa kwa Kindiki Kithure kama naibu spika wa senate ni jambo linalokubalika kwani seneta huyo alikuwa amemkaidi kiongozi wa chama chake .siku ya ijumaa maseneta 54 kati ya 67 walipiga kura kumuondoa Kindiki kutoka wadhifa huo .

Wale waliopiga kura kumuokoa Kindiki ni   Kipchumba Murkomen wa  Elgeyo Marakwet, Susan Kihika wa  Nakuru, Samson Cherargei wa Nandi, Aaron Cheruiyot wa  Kericho, Christopher Lang'at wa  Bomet na Mithika Linturi wa Meru.Kindiki  wakati mmoja alikuwa ametajwa kama anayeweza kuwa mgombea mwenza wa naibu wa rais William Ruto wakati wa uchaguzi mkuu wa 2022 na kuondolewa kwake kama naibu spika wa senate ni pigo kwa mrengo wa DP

Munya amesema hatua ya kuondolewa kwa  Murkomen na susan Kihika katika uongozi wa senate ni dhihirisho kwamba rais Kenyatta  analenga kukinadhifisha chama cha Jubilee ili kuboresha ajenda yake ya maendeleo na usimamizi ufaao  wa shughuli za serikali .

Nafasi zao zilichukuliwa na Samuel Poghisio wa West Pokot  na seneta wa Murang’a Irungu Kang’ata,

Munya  amesema kila mtu anafaa kuubeba msalaba wake  na kufuata mkondo anaotaka kinara wa chama cha Jubilee na  Mkuu wa serikali ,Uhuru Kenyatta