Rais Donald Trump wa Amerika ameondolewa makosa yote katika mchakato wa kumwondoa madarakani kupitia kura ya senate katika kufikisha tamatai utaratibu wa kumuonyesha mlango kabla ya kumalizika kwa kipindi chake afisii .Senate, inayoongozwa na wanachama wengi wa chama cha Trump cha run Republican, ilipiga kura kumpata bila hatia rais huyo kwa kura 52 dhidi ya 48 kuhusu kutumia vibaya maamlaka yake kura 53 kwa 47 kuhusu madai ya kuzuia Congress kufanya kazi yake .
Wanachama wa Democrats walimshtaki rais Trump disemba kwa madai ya kuishinikiza Ukraine kumchunguza anayeweza kuwa mpinzani wake katika uchaguzi ujao wa urais ili kumchafulia jina kabla ya kura.
Katika kura hiyo ya kihistoria Senate iliamua kutomuodnoa afisini Bwana Trump ambaye anagelazimika kumkabidhi maamlaka makamu wake Mike Pence endapo mashtaka dhidi yake yangeidhinishwa . Trump anayetafuta muhula wa mwisho na wa pili Novemba tarehe 3 amekuwa akikanusha kufanya kosa lolote . Amekuwa akidai kwamba wanachama wa democrat wana hila dhidi yake na hiyo basi kuwa na uchu wa kutafuta kila fursa ya kumuondoa afisini .