Duru zaarifu kwamba polisi waliamua kufanya oparesheni katika eneo hilo la burudani baada ya washukiwa kadhaa kukamatwa wakiwa na sachet za cocaine katika maeneo mbali mbali ya Nairobi . Baadhi ya washukiwa waliokamatwa ndio waliomhusisha Akinyi na mtandao wa kusambaza dawa hizo za kulevya . Akinyi sio mgeni wa sakata kama hizo kwani mara ya mwisho alipokamatwa mwaka wa 2015 alipatikana na podari iliyoshukiwa kuwa cocaine .Baadaye aliachiliwa huru pamoja na washukiwa wengine watatu .
Mwaka wa 2013 Akinyi na mbunge Budalangi Raphael Wanjala walikamatwa na polisi katika barabara kuu ya Nairobi kwenda Namanga katika eneo la Isinya kwa madai ya ulanguzi wa dawa za kulevya .Baadaye waliachiliwa huru waliposisitiza kwamba walichokuwa wamebeba ni unga wa mahindi ulioagizwa kutoka Tanzania .Wanjala na Akinyi, ambao wanadaiwa kuwa wapenzi pia wamewahi kuzuiliwa nchini India mwaka wa 2008 walipopatikana na shilingi milioni 7.59 ambazo hawakuwa wameeleza maamlaka walikozitoa .Waliachiliwa huru baada ya maamlaka za Kenya kuingilia kati.
Akinyi na mumewe waliyetengana naye raia wa Nigeria Anthony Chinedu wamehusishwa na mtandao wa usafirishaji wa dawa za kulevya na pia wamewahi kugonga vichwa vya habari kwa kuzozania eneo la burudani la Deep West lenye thamani ya mamilioni ya pesa .Baadaye Chinedu alirejeshwa nchini Mwake .