Not Again! Rais Trump ashtumiwa tena kwa ubakaji

Mwandishi mmoja  wa makala katika jarida la   mitindo la Elle  amedai kwamba Rais wa marekani Donald Trump alimdhulumu kimapenzi  katika eneo la kubadilisha nguo la duka moja la mavazi  huko New York ,miongo miwili iliyopita .E Jean Carroll ametoa madai hayo katika   kitabu  alichokichapisha  siku ya ijumaa .

Trump  amejibu madai hayo kupitia Twitter  kwa kusema kwamba hajawahi kukutana na  E Jean Carroll,  na kwamba tukio hilo ‘halikuwahi kufanyika’. Kulingana na Carrol ,dhulma hiyo ilifanyika  kati ya mwaka wa 1995 au 1996  wakati Trump alipokuwa mdau kumbwa katika sekta ya ujenzi wa majumba  naye mwandihsi  akiliandikia jarida moja kando na kuwa mtangazaji wa kipindi cha televisheni .

Ufichuzi huo  uliotolewa katika kitabu cha Carrol  kilichochapishwa ijumaa kinamfanya kuwa mwanamke wa 16 kudai kudhulumiwa kimapenzi na rais huyo wa Marekani .Carroll ambaye sasa ana umri wa miaka 75,  amesema alikutana na Trump katika duka la nguo la  Bergdorf Goodman  huko Manhattan  walipokuwa wote wakinunua nguo . Amesema mwanzoni mazungumzo yao yalikuwa ya kirafiki  wakati Trump alipotaka ushauri wake kuhusu vazi la ndani  alilotaka kumnunulia mwanamke ambaye hakumtaja . Kisha  kwa utani walipendekeza kwamba  kila mmoja wao angelijaribu kuvalia vazi hilo.

" Pindi mlango wa chumba cha kubadilisha kilipofunguka , alinijia  kwa nguvu na kunisukuma ukutani,nikapiga kichwa changu kwa uchungu  kwenye ukuta kisha akaiweka mido yake kwenye yangu ’ Carrol ameandika . Baada ya kumbana ukutani Carrol anasema Trump aliendelea kumfunua vazi lake ,akajifungua  long’i kisha akamwingilia kutumia uume wake-wakati wote Trump alikuwa bado amevalia nguo zake hadi Carrol alipomudu kumsukuma na kisha kukimbia kutoka chumba hicho cha kubadilisha .Carroll  hakuripoti kisa hicho kwa polisi kwa sababu anasema alihofia matokeo yake .

Ameandika kwamba aliogopa kujitokeza hadharani kusema kilichotokea kwa ajili ya kuogopa ‘kupokea vitisho vya kuuawa ,kutoroshwa kutoka kwake,kupuuzwa au kupakwa tope’