ROGUE BLOGGER:Mwanablogu Cyprian Nyakundi akamatwa kwa hila ya kupunja shilingi Milioni 17 kutumia vitisho

nYAKUNDI
nYAKUNDI
 Makachero wamemkamata mwanablogu Cyprian Nyakundi na mshukiwa mwingine  Emmanuel Nyamweya Ong'era  kwa njama ya kutaka kupokea shilingi milioni 17   ili kuondoa chapisho la mtandaoni la kumharibia mtu jina .

Wawili hao tayari walikuwa wameshapokea shilingi milioni 1 kama sehemu ya malipo hayo .

https://twitter.com/DCI_Kenya/status/1219238606184894464

Inadaiwa wawili hao waliitisha kiasi hicho cha pesa kama  sharti la kuondoa chapisho hilo kutoka kwa blogu inayomilikiwa na Nyakundi . wawili hao watazuiliwa na polisi hadi Jumanne tarehe 21 watakapofikishwa kortini . Pesa hizo pia zilipatikana  na zitatumiwa kama ushahidi .