Makachero wamemkamata mwanablogu Cyprian Nyakundi na mshukiwa mwingine Emmanuel Nyamweya Ong'era kwa njama ya kutaka kupokea shilingi milioni 17 ili kuondoa chapisho la mtandaoni la kumharibia mtu jina .
Wawili hao tayari walikuwa wameshapokea shilingi milioni 1 kama sehemu ya malipo hayo .
https://twitter.com/DCI_Kenya/status/1219238606184894464
Inadaiwa wawili hao waliitisha kiasi hicho cha pesa kama sharti la kuondoa chapisho hilo kutoka kwa blogu inayomilikiwa na Nyakundi . wawili hao watazuiliwa na polisi hadi Jumanne tarehe 21 watakapofikishwa kortini . Pesa hizo pia zilipatikana na zitatumiwa kama ushahidi .