Peter Gatimo ambaye alifikishwa kizimbani akiwa amevaa tu kaptula yake ya ndani alielezea kuwa alikamatwa ijumaa na kuagizwa kuvua nguo zote na afisa ambaye alikuwa anasimamia kituo hicho lakini jina lake halikutajwa.
Gatimo alidai kuwa maafisa hao hawangeweza kumfikisha mahakamani siku ya jumatatu kama inavyotakiwa kisheria kwani walidai kuwa hawangeweza kupata nguo yake. Gatimo aliongeza kuwa alipewa nguo zingine avae ambazo hazikuwa zinamtoshea lakini alikataa kuzivaa.
Wawili hao walifikishwa mbele ya hakimu Angelo Kithinji ambaye alimuagiza afisa wa upelelezi kuuliza OCS kuhusu tuhuma hizo mbili tofauti ya wizi wa nguo za wafungwa.
Gatimo anashtakiwa kwa wizi na vurugu mnamo septemba 12 katika kituo cha basi OTC, kando ya barabara ya racecourse jijini Nairobi.