Tisa wametemwa nje baada ya kukosa kuafikia vigezo vya chama hiki. Idadi ya wagombea 23 waliojaza fomu imepungua hadi 11 sasa ili kujitayarisha kwa mchujo wa chama utakaofanyika Agosti 31 kabla ya uchaguzi utakaofanyika Novemba 7.
Soma hapa:
Majina yaliyowasilishwa ni ya Christone Odhiambo almaarufu kama DJ Kris Darlin, Peter Ochieng, Tony Ogola Sira, Reuben Ojijo and Stephen Okello.
Bernard Otieno, Eric Ochieng, Brian Owino, John Otieno, Benson Musungu and Patrick Lumumba Owade ni majina pia ambayo yapo kwenye orodha.
Chama tawala cha Jubilee pia kinatarajiwa kutoa mgombeaji wao baada ya shinikizo katika chama hicho. Rais Kenyatta ambaye ni kinara wa chama hicho hakutaka wawasilishe mgombeaji ila baada ya wanachama kushauriana wakaamua kufanya hivyo.