Oh No! Wanariadha 2 wa Kenya wapigwa marufuku .

Chepkurui
Chepkurui
  Wanariadha wawili wa Kenya  wamepigwa marufuku dhidi ya kushiriki  mashindano ya riadha baada ya kupatikana na makosa ya kutumia dawa zilizoharamishwa . Bingwa wa mwaka wa 2014 wa Glasgow Commonwealth na  bingwa wa afrika  wa mbio za mita 10,000 Joyce Chepkirui na mwanariadha wa masafa marefu John Jacob Kibet Kendagor ndio wakenya hivi punde kupigwa marufuku .

Chepkirui,  ambaye pia alishinda mbio  za  marathon za Amsterdam na Honolulu marathons  mwaka wa 2015  kando na kumaliza wa 10 katika Boston marathon mwaka huo  amepigw amarufuku Athletes Integrity Unit (AIU)  baada ya kasoro kutokea katika vipimoa vya sampuli ya kumtambua yaani Athletes Biological Passport (ABP).

Chepkirui,  aliyeshinda medali ya fedha katika  mashindano ya ubingwa wa afrika mwaka wa 2011 katika mbio za mita 1500  na fedha tena katika mbio za nyika  za afrika mwaka wa 2012  hajashiriki mahsindnao yote mwaka huu .Chepkirui,  aliyekulia katika   wilaya ya Buret huko Rift valley alianza kukimbia katika ulingo wa kimataifa  mwaka wa 2007 katika mashindano ya ubingwa afrika kwa chipukizi  ambapo alimaliza wa tano katika mbio za mita 1500.