Chepkirui, ambaye pia alishinda mbio za marathon za Amsterdam na Honolulu marathons mwaka wa 2015 kando na kumaliza wa 10 katika Boston marathon mwaka huo amepigw amarufuku Athletes Integrity Unit (AIU) baada ya kasoro kutokea katika vipimoa vya sampuli ya kumtambua yaani Athletes Biological Passport (ABP).
Chepkirui, aliyeshinda medali ya fedha katika mashindano ya ubingwa wa afrika mwaka wa 2011 katika mbio za mita 1500 na fedha tena katika mbio za nyika za afrika mwaka wa 2012 hajashiriki mahsindnao yote mwaka huu .Chepkirui, aliyekulia katika wilaya ya Buret huko Rift valley alianza kukimbia katika ulingo wa kimataifa mwaka wa 2007 katika mashindano ya ubingwa afrika kwa chipukizi ambapo alimaliza wa tano katika mbio za mita 1500.