Mhudumu mmoja wa bodaboda wa kampuni ya kutisha huduma za usafiri kutumia mfumo wa simu amekamatwa siku ya alhamisi usiku na maafisa wa DCI baada ya kumwibia ,kumbaka na kumuacha mteja wake .
Mshukiwa aliyetambuliwa kama Dennis Wekesa mwenye umri wa miaka 27 alimfanyia unyama huyo mwanamke mzungu kabla ya kutoroka na vifaa vyake na kumuacha katika kichochoro kimoja . Mwathiriwa alikuwa ameitisha huduma za pikipiki kwenda mtaani kileleshwa katika jumba la Anahita Appartments eneo la parkalands .
" Walipokuwa wakienda parklands ,mhudumu wa boda boda alishuka na kumbaka mteja wake na kisha kumpokonya kila kitu na kuizima simu yake’ DCI imsema
Alikamatwa na maafisa wa ktengo maalum cha kuzuia uhalifu katika eneo la Gachie . Mwathiriwa amehsapokea matibabu hospitalini na kuruhusiwa kwenda nyumbani. Wekesa atafikishwa kortini pindi uchunguzi wa tukio hilo utakapokamilishwa.