Papa Francis kuruhusu wanaume waliooa kuwa mapadri

papa francis
papa francis

Maaskofu wa kanisa katoliki wamepiga kura kuruhusu wanaume waliooa kuwa mapadri katika eneo moja la pembezoni ili kuweza kupata mwanya wa kuhubiri katika eneo la Amazon.

Hatua hiyo imekuja mara baada ya Papa Francis kutoa ombi kuwa ni vyema kutoa ruhusa kwa wanaume walioa kuwa mapadri kwenye sehemu maalum katika eneo hilo la Amazon.

Eneo ambalo waumini wengi wanaotaka kushiriki misa na kupokea mkate wa komunio hawaonagi mapadri kwa zaidi ya miezi kadhaa na muda mwingine hata miaka.

Amesema yeye na washiriki wengine wanaojulikana kama 'synod' wapo wazi kwa mawazo ya kutafuta njia mpya itakayosaidia kusambaza imani hiyo.

Watahitajika kupata wanaume wanaoheshimika na kulingana na stakhabadhi hizo watafanya kazi katika jamii wanazotoka.

Maaskofu wa Marekani Kusini wamepigania juhudi hizo ili kukabiliana na upungufu wa mapadri katika eneo hilo.

Lakini wakosoaji wamedai kuwa papa anapaswa kuhamasisha mapadri wasioe, ingawaje katika karne ya kwanza ya kanisa, mapadri waliruhusiwa kuoa, na karibia mapapa wote wa mwanzo walikuwa wameoa.

Vilevile kuruhusu wanaume walioa katika sehemu za Amazon ambazo zinakabiliana na ukosefu wa mapadri, kutaenda kinyume na sheria za kikatoliki ambazo zimekuwepo kwa miaka kadhaa sasa.

Kwa sasa papa anaruhusu wanaume walioa kuwa mapadri katika makanisa ya mashariki ya kati pekee.

Upigaji kura ukiwa unafikia ukingoni huko Vatican kutokana na uhaba wa mapadre ili mapendekezo hayo yaanze kufanya kazi rasmi.

Wengi wakiwa wanahofia mabadiliko hayo katika kanisa kwa kuanzisha utaratibu mpya katika kanisa.

Kura zimechukuliwa kwa kipindi cha wiki tatu,kwa maaskofu 180 wa mjini Rome.

Wakiwa wanaangalia majukumu ya wanawake katika kanisa na namna mazingira yatakavyoweza ruhusu.Kanisa katoliki ni taasisi kongwe ya kidini ambayo imekuwa na historia kwa zaidi ya miaka 2000 iliyopita huku ikiwa na mabilioni ya waumini.

Huku inakadiriwa kuwa karibu 85% ya vijiji huko Amazon haviwezi kusherehekea Misa kila wiki kwa sababu ya uhaba huu na wengine huonana na makuhani mara moja tu kwa mwaka.

-BBC