PATANISHO: Bibi yangu anatetea mpango wake wa kando

Paul aliomba apatanishwe na mkewe bi Elizabeth akidai kuwa wawili hao walikosana baada yake kumpiga mpango wa kando.

Akieleza kisa hicho, bwana Paul alidai kuwa wawili hao walikuwa wametengana kwa mda na kila mmoja akaanza uhusiano wa kando na baada yao kurudiana, aliyekuwa mpango wa kando wa mkewe hakusita kumfuata.

Jambo hilo lilimkera haswa baada yake kumtumia picha za mkewe kwa mtandao wa Whatsapp na alipopatana naye alimpa kichapo cha mbwa, jambo ambalo halikumfurahisha mkewe.

Kwa hasira na kero kuu, Paul alimfukuza Elizabeth.

Soma usimulizi wake.

Tulikuwa tumekosana hapo mbeleni na tuka separate kidogo. Katika hali ya ku separate akapatana na mtu mwingine halafu tukaja tukarudiana. Baada ya kuishi naye yule jamaa bado alimfuata na baada ya kuzungumza na mke wangu tukamaliza hayo maneno, na nikampigia yule jamaa na nikamkanya.

Sasa hakuacha na akaendelea kumfuata na ikafika mahali akaanza kutuma picha za bibi yangu kwa Whatsapp na hiyo kitu iliniuma sana.

Nikamwambia bibi yangu anipatanishe na yule jamaa, tukazungumza na nikakasirika zaidi nikampiga yule mwanaume na bibi yangu nikama lile jambo halikumfurahisha na akaanza kumteta yule mwanaume na kwa machungu ikabidi nimfukuze mke wangu. Aliondoka na kwenda kwao nyumbani na hawazungumzi na yule jamaa.

Wawili hao wana watoto wawili mmoja alimuoa naye na wamekuwa kwa uhusiano wa miaka minane.

Bi Elizabeth naye alidai kuwa Paul alimtumia fedha za kununua sare za shule lakini pindi tu zilipofika akazirudisha. Alisisitiza mumewe ana madharau sana na hadai kurudiana naye.

Hata hivyo alimuomba ashughulikie watoto huku akimpa mda.

Pata uhondo wote.