PATANISHO: Enda uite wanaume wako wa barabarani uwapikie

Mama Vale alituma ujumbe akiomba apatanishwe na mumewe baba Vale.

Alianza kunisumbua kuanzia mwaka jana mwezi wa kumi na mmoja, sasa juzi tarehe ishirini na mbili ikawa kuna mwanamke alikuwa anapiga simu.

Nikaangalia na nilipomuuliza ni nani alidai hayo maneno ya message na simu yasinisumbue sana. Nikamueleza kama chenye anafanya ni kizuri aendelee. Alielezea mama Vale.

Kesho yake akaenda kazini na hakurudi, sasa nikajijazia ni yule mwanamke. Sasa wiki mbili baadae hali kwa nyumba, nikimwekea maji kwa bafu haogi. Kumuuliza kwenye hula akaniambia niende nilete wanaume wangu ninaowasimamisha barabarani ili wale kile chakula." Aliongeza mama Vale.

Wawili hao wamekuwa kwa ndoa ya miaka minane na wana watoto watatu.

Alipopigiwa simu baba Vale alicheka akidai yeye hana maneno huku akimkemea kabla ya kukatiza mawasiliano.

&feature=youtu.be