PATANISHO: James Alalamikia Kunyang'anywa Mke Na "Jamaa Wa Maziwa"

patanisho.
patanisho.

Siku ya Jumatano tarehe 7/12/2016 bwana James mwenye umri wa miaka 26, kutoka maeneo ya Thome aliomba apatanishwe na mkewe Elizabeth 24, ambao walikosana majuma mawili yaliyopita.

Wapendwa hao wawili wana mtoto mmoja ambaye James alimuoa mkewe naye na wawili hao wamekuwa pamoja tangia mwaka wa 2013.

Kulingana na bwana James, siku moja mkewe alielekea kazini lakini hakurudi. Alipompigia simu mkewe alimwambia kuwa  asisumbuliwe na kukata mawasiliano kati ya wawili hao.

Baada ya hayo, James alihamia chumba kingine katika ploti hiyo hiyo kwa uchungu mwingi na wakti mkewe aliporejea nyumbani, wawili hao waligawana mali na la kuchesha zaidi ni kuwa wawili hao walipatana asubuhi ya leo huku James alipokuwa akielekea msalani naye Elizabeth akielekea bafuni.

Isitoshe James alisema kuwa chanzo kuu cha wawili hao kutengana na kuzua shida chungu nzima, ni mwanaume mmoja aliyekuwa akimletea mkewe maziwa. Hapo alishuku huenda jamaa huyo na Elizabeth wana uhusiano kwani walipotengana, jamaa huyo alianza kumletea mkewe maziwa hadi kwake nyumbani.

Alipopigiwa simu Elizabeth ambaye ni shabiki wa Patanisho alikiri kuwa tabia za bwanake kama kutokuwa mkamilifu na kuwa mwizi ndizo chanzo cha wawili hao kukosana.

"Ana tabia za wizi kwa ploti ananiletea aibu kwa nyumba. Hanunui chochote hata chakula, patipati hamna chochote anafanya ispokuwa kulipa kodi. Niliporudi nyumbani kutoka matembezi nilipata James amehama na singemlazimisha." Alieleza Elizabeth.

"Jamaa wa kuuza maziwa ni rafiki yangu na ndiye natarajia anioe. Nilianza uhusiano naye kwa sababu yeye alikuwa ananitunza, asiponisaidia mimi na mtoto wangu tunalala njaa. Bwanangu alikuwa anamtuma mtoto wetu chapati ala huku mtoto akimtizama." Alieleza zaidi bi Elizabeth huku akisema kuwa hataki maneno yake hata kidogo.

Bwana James aliposkia hayo yote alitoweka na kukata mawasiliano. Do!

Skiza uhondo kamili.

&feature=youtu.be