PATANISHO: Kakangu Alimkashifu Dada Yetu Kuwa Ni Illuminati Na Alimuua Ndugu Yetu

Mutonyi alituma ujumbe akiomba apatanishwe na dadake Lydia ambaye walikosana sana kwa kumtusi kupitia ujumbe wa simu, miaka miwili iliyopita.

Tangia kisa hicho wawili hao hawajawahi zungumza.

"Tulikosania juu ya mtoto wake kijana, ambaye alikuwa anaishi naye. Alikuwa kijana kichwa ngumu sana na dadangu akang'ang'ana sana kumsomesha na siku moja akamlipia karo ya shilingi elfu arobaini. Kumbe kijana alidanganya kuwa ameenda shuleni lakini hakwenda. Sasa dadangu akanieleza nielekee kwake nimsaidie kuzungumzia kijana.

Basi kijana bado aliendeleza utukutu wake na hapo akamwambia kuwa afunganye virago vyake arudi kwa babake. Hapo niliona haifai kwani babake hakuwa na uwezo na katika harakati ile tukatusiana na nikamtusi vibaya sana." Alieleza bwana Mutonyi.

Nilimuambia kuwa alifanya ndugu yetu mmoja afariki ili anitawale. Nilijaribu kumuomba msamaha lakini siku moja alingangana sana nami karibu animalize." Aliongeza Mutonyi.

Alipopigiwa simu, Lydia hakuwa karibu ila dadake ndiye aliye jibu simu zetu.

"Mutonyi alipokosana na dada yetu alimtumia ujumbe akisema kuwa aliingia Illuminati na hapo akaua ndugu yetu. Huyu jamaa ana matusi mbaya kwani pia mimi huwa ananirushia matusi lakini huwa namuangalia tu.

Dadangu naye alikasirishwa sana na hayo kwani anafanya kazi ngumu sana." Rebecca.

"Naomba mnisamehe Rebecca kwani hayo yote nilikuwa nafanya nikiwa mlevi. Nilikuwa na tabia za ulevi na nimeokoka sasa hivi." Alijitetea Mutonyi.

Pata uhondo kamili.

&feature=youtu.be