Patanisho: Mama mkwe hataki nikae na bibi yangu

Ali, alituma ujumbe akisema kuwa walikosana na mkewe mwezi wa Mei mwaka huu na hadi wa leo hajarudi. Isitoshe wawili hao wakizungumza mkewe humwambia aende kwao nyumbani lakini mamake hadai maneno yake.

"Unajua hii ndoa, mahari yangekuwa yamelipwa kitambo sana, lakini sasa wakati ambapo mahari nimetayarisha na niko tayari kutuma watu kwao, mamake analeta vurugu, msichana pia sasa inaleta shida. Lakini nampenda Christine." Alijitetea bwana Ali.

Wawili hao wamekuwa kwa ndoa ya miaka sita na wamejaliwa na watoto wawili ambao wako nyumbani kwa Christine.

Nilifuatilia mbona mama analeta shida kwani ilifika mahali mamangu na mamake walizozana kwani mahali nimeoa ndio mahali dadangu ameolewa. Sasa walipokosana wanataka pia mimi nikosane na mke wangu." Aliongeza.

Alipopigiwa simu, mama mkwe alisema kuwa yeye hana shida na Ali akidai kuwa hana ubaya wowote kwani bado hajamjua licha yake kuzaa watoto wawili na mwanawe.

"Hata sijamjua na amezaa watoto wawili na mke wangu, tena alimtoa shuleni." Alieleza.

Pata uhondo kamili.