PATANISHO: Mke wangu alimwaga nyama na akakula fare!

Kimani, 36, kutoka Narok, aliomba apatanishwe na mkewe bi Purity, 33, akisema wawili hao walikosana mwaka wa 2017 baada ya kuwa ndani ya ndoa ya miaka minne akiongeza kuwa wakti huo alikuwa mja mzito.
"Tulikosana kwa sababu ya siasa za familia yetu na naskia kuwa sasa hivi yuko Murang'a na maeneo ya Thika." Alisema.

Aliongeza,

Aliniambia kuwa nilikuwa napendelea wazazi sana, wakati huo alikuwa mja mzito na nilirudi na nyama nyumbani. Alikuwa amekasirika na nilipopika akamwaga ile nyama na nikakasirika na kumzaba kofi."

Kimani anasema kesho yake bi Purity aliondoka na tangia wakti huo hawajawahi suluhisha kesi hiyo.

Huwa tunazungumza na nikamtumia nauli ila hajawahi rudi nyumbani licha ya kuniahidi mara kwa mara.

Alipopigiwa simu alisema kuwa "Mtu akipenda mtu hujipenda kwanza, wewe una tabia ya kuskiza mamako na ukumbuke ulitoka kwa mamako na boma lako sio la mamako." Alisema Purity.

Maji yakimwagika hayazoleki, familia yake ni wale wa kuchocha wakiona tunaendelea vyema naye anawaskiza licha ya kumkanya. Nilimsamehe kitambo ila mambo ya ndoa niliwacha, wacha sasa nilee watoto kwanza."

Purity anasema kabla ya kuondoka, nyumba aliyochangia pakubwa kwa ujenzi mamake alimshauri Kimani atafute mwanadada aliyepata naye mtoto aje waishi naye.