PATANISHO: Mume Wangu Alidai Kuwa Nilimuekea Sumu Kwa Chakula Chake

Ann 27, alituma ujumbe akiomba apatanishwe na mumewe bwana Julius mwenye umri wa miaka 27 ambaye wameishi pamoja kwa mda wa miaka mitano.

"Ilikuwa mwezi wa tano na nilipata ujumbe kwa simu yake akiwa ameandikia msichana mwingine akimueleza anavyompenda. Kumuuliza huyo ni nani analeta ugomvi na mambo yakabadilika ghafla.

Mara anatufungia nje ya nyumba na mtoto tunalala nje. Ikabidi nimeelekea nyumbani na hapo alikuwa anapiga simu akidai kuwa nipatie mtoto simu azungumze naye bila kukumbuka kuwa mtoto hawezi zungumza. Mda mchache baadaye akaanza kunigombanisha baada ya kugundua kuwa nimeanza kufanya vibarua, kwani alikiri kuwa sifai kumwacha mtoto mdogo kwa nyumba na saa hizo hajaniwachia fedha.

Juzi tu tulikuwa naye kwa nyumba tukala pamoja na sasa akala hicho chakula jioni. Lakini akanipigia simu siku iliyofuata akidai kuwa nilimuekea dawa kwa chakula na kuwa nataka kumuua. Hapo akadai niondoke kwake hataki kuniona." Alijieleza bi Ann.

Bwana Julius alikatiza mawasiliano yetu pindi tu alipogundua ni Redio Jambo kabla ya kujibu simu yetu.

"Niliomba mtoto mpaka kwao lakini hawajanipatia si waniletee mtoto, kurudiana kama bibi na bwana nayo siwezi kwani mimi nina haja ya mtoto." Alisema Julius.

Pata uhondo kamili.

&feature=youtu.be