PATANISHO: Mume wangu hata nguo za ndani hanishughulikii

Mama Manu alituma ujumbe akiomba apatanishwe na mumewe bwana George, akidai kuwa wawili hao walikosana mwaka uliopita na hadi wa leo hawaelewani.

Kulingana na mama Manu, "Hatuzungumzi licha ya kuishi katika nyumba moja, hanishughulikii kama mke wake na hata tendo la ndoa sipati." Wololo.

"Tumekuwa tu tunasumbuana sumbuana kwa nyumba na hanishughulikii hata kidogo. Mimi ni house wife na bado sijapata kazi, huyo mwanaume hata nguo ya ndani hajawahi ninunulia kwani mavazi ninayo vaa ni ya dadake ambayo aliwacha kwetu." Aliongeza akisema kuwa mumewe akitoka hurudi akiwa amelewa chakari.

Nishawahi zungumza na watu wao lakini kuna kitu niliambiwa nikakasirika. Babake aliniambia kuwa mlevi ni mlevi tu na akasema like father like son. Babake hata ndio mlevi kupindukia." Alisema.

Wawili hao wamejaliwa watoto wawili.

Bwana George alijibu simu kwa mda mchache tu kabla ya kukata mawasiliano na kuzima simu yake.

Hata hivyo, mama Manu alimuomba mumewe arejee nyumbani na ampee mapenzi tele kwani yuko 'dry spell'.

Mwanamke sio skirt mwanamke ni mapenzi, anaweza ona nimevalia sketi anadhania niko sawa. Siko sawa kwani mambo ya kushiriki mapenzi ni ndoto kwangu.