Patanisho: Naishi kwa ndoa nikiogopa mme wangu

Je, ndoa kama hizi ni sawa ama vipi? Unapata kwamba mtu anaogopa tuu, na si mwanamke peke yake. Utapata mwanaume mwingine pia wanaogopa wake zao,

Ni mapenzi ya aina gani haya? Nini huwa inaleta woga katika uhusiano y akimapenzi? Je, ni mapato inayo changia haya matatizo?

Jane aliomba apanishwe na mme wake Mwangemi walikosana Wednesday, alitoroka usikua na watoto akanifuata stage, akanipiga vibaya sana. Naomba umpigie umuulize kweli ananipenda au niende nyumbani.

Alieleza hali yake kwa Gidi kupitia simu:

'Ilikuwa mambo ya pesa. Nilimwambia anipee pesa kidogo  akaniambia saa hizi sina lakini angalia kwa kiatu utaona shillingi hamsini. Sasa nikajiuliza kwanini aninifichia pesa. Alipokuja jioni nikamuuliza, ndio hapo akakasirika. Kisha baadaye akaniambia nirudi nyumbani, na hadi sasa haniongeleshi. Nampenda na ningependa hii ndoa yetu iendelee.

Kila mmoja amenuna pale. Inaonekana ni mzee mkali na Jane anamuogopa.

Kwa bahati mbaya, bwana Mwangemi hakupokea simu kwa mara ya pili. Ilibidi Gidi apatie wanajambo ushauri.

Skiza kanda ujue kama Jane alipata usaidizi kupitia wanajambo, au la: