PATANISHO: Nili promote mpango wa kando kuwa mke

Kelvin alituma ujumbe akiomba apatanishwe na mkwewe bi Eunice, ambaye walikosana na kutengana mwaka mmoja uliopita.
"Nilikuwa na mpango wa kando ambaye nilimuoa kama mke wa pili na hapo ikaleta shida kwa ndoa. Mke wangu akakasirika na hapo nikawachana na mke wa pili lakini tukakosa maisha ya kuaminiana.

Yeye akitoka haniamini nami akitoka simuamini na ilipofikia mwezi wa tano akaondoka na kuniachia watoto." Alisimulia Kelvin.

Anadai wawili hao hulea watoto pamoja lakini hapendelei watoto kuishi mahala kwingine lakini kila anapompigia mkewe bado ana ugumu wa kurudi.

Wawili hao wamekuwa kwa ndoa ya miaka kumi na wawili hao walioana wakiwa na umri mchanga sana.

Alipopigiwa simu bi Eunice alidai kuwa mumewe amechelewa kwani walikuwa wamemaliza kutatua maneno yao.

"Kwa uamuzi wangu ni eti tulikuwa tumezungumza, kwanza mahala amekosea ni kuwa ameenda kunianika Radio Jambo." Alisema Eunice akisisitiza kuwa watoto watalea pamoja lakini hatorudiana naye.