PATANISHO: Nilifisia mwanamke mwingine bibi akaniacha

Bwana Kai alituma ujumbe akisema alikosana na mpenziwe bi Muthoni kutoka mwaka jana.

"Kuna dem flani ambaye nilikuwa navizia vizia na sasa bibi yangu akaja akajua na ikabidi nimfiche, lakini sasa alikuwa amejua ukweli na hata alimuuliza na msichana akadhibitisha.

Sasa bibi yangu akakasirika na akaenda halafu kuna shida nyingine kwani mama yangu hakuwa anampenda na kuchanganya mawili akaondoka lakini mimi bado nampenda, kwani yeye ndio mama wa watoto wangu." Alieleza Kai akidai kuwa wawili hao wamejaliwa watoto wawili.

Isitoshe mwanadada hakuwa ameingia box kwani bado ulikuwa mchezo wa paka na panya bado tulikuwa tumefukuzana, kwanza sikuwai huyo mwanamke na hata staki kumuona kabisa.

Wawili hao wana miaka ishirini na minne.

Alisema tangia aondoke walikuwa wakizungumza kwa mda wa miezi miwili lakini mkewe alikujia watoto wao wakati Kai hakuwa nyumbani.

"We nakuuliza shida yako nini? Si nilikuambia uwache kunisumbua ama akili yako changa sana haiwezi shikanisha? Nilikuambia uwache kunisumbua, skiza na kama umetafuta mahali pa kwenda ukakosa ukaona unipigie simu ufanye heshima yako unaskia?" Alitema Muthoni  kabla ya kukata mawasiliano.

Wacha nikuambia mimi kwa maoni yangu kama wanaume design ni hiyo, wacha basi mtu ajikalishe juu kama mwanaume utamshika mtu anaenda hana time yako unamkuta kwa nyumba za wanawake wengine na anaruka, anaenda huko nje akisema hana bibi anataka kuoa. Mimi nilimwambia awache kunisumbua sina time yake. Aliongeza akisema hataki kuskia sauti yake.

Pata uhondo kamili.