PATANISHO: Utangoja Miaka Mitano Na Kama Una Haraka Tafuta Mke Mwingine!

Kepha alituma ujumbe akiomba apatanishwe na mkewe bi Purity akidai ndoa yake imesambaratika baada ya wawili hao kukosana miezi mitatu Sasa.

Tulikosana na mke wangu siku moja nikitokea kazini. Mwanaume mmoja akanipigia simu akidai kuwa nasumbua mke wake kwa simu. Kumuuliza mke wangu akadai haijui ile nambari.

Siku moja mtoto wangu akaniletea picha akilia kuwa mamake anafanya tabia mbaya. Kwa ile picha mke wangu alikuwa ameshikana na Mwanaume mwingine visivyo, Kumuuliza mke wangu yule ni Nani akanijibu "Wewe unaona kama ni Nani?"

Hapo nikaumwa na nikampiga na baada ya kuzungumza naye alikiri kuwa yule ni mfanyi kazi mwenza na kuwa nafaa kungoja miaka mitano ili arudi na kama nina haraka nioe mke mwingine.

Pata uhondo kamili.

Soma patanisho zingine

&feature=youtu.be