PATANISHO: Wazazi wa bwanangu huniona mimi kama msherati

Bwana Meshack alituma ujumbe akiomba apatanishwe na mkewe. Alidai walipokosana mkewe aliondoka wiki iliyopita na kuelekea Mombasa na kila mara hukatisha mawasiliano kati yao wawili.

Wawili hao wamekuwa kwa ndoa ya miaka kumi na mitatu na wamejaliwa watoto wawili.

"Nilitoka kazini nikapata amefunga mlango na kutoa vitu kadhaa na kuondoka.

Mke wangu alidhania nina mipango ya kando baada ya kupata number kwa simu yangu na nikamueleza kuwa ni ya supervisor wangu. Lakini alisema kuwa ni mfanyikazi mwenzangu na tuna uhusiano naye." Aliongeza Meshack.

Mercy alipopigiwa simu alidhibitisha kuwa yuko Mombasa kazini.

"Nimevumilia sana na hata kama mtu husema nilikuwa nataka kuolewa ni mimi. 2011 aliniwacha kwao Kakamega na kwenda kazini alipoondoka mamaake na ndugu yake walinipa kichapo cha mbwa.

Nilishughulikiwa na pastor na wazazi wangu walinipata nikiwa hospitalini Kakamega. Waliponipeleka nyumbani, bwanangu akawajibu babangu na babu akiwaambia kuwa msichana wengi ndio mbaya ndiye aliye piga mamangu na babangu. " Alieleza Mercy ambaye licha ya hayo yote alirudi kwa bwanake.

Kurudi kwake akaendelea kunitusi, madharau na kutembea na wanawake hadharani bila kusahau husema kuwa mimi hununuliwa pombe na kulazwa na wanaume. Isitoshe yeye huwa hashughulikii watoto na siwezi ng'ara au kusalimia majirani kwani hudai hao ni bwana zangu." Aliongeza.

Pata uhondo kamili.

&feature=youtu.be