Patanisho:Bwana akosana na shemeji!Je nani atamsaidia kuremjesha mke wake

Mengi hutokea katika ndoa na hivi leo katika kitengo chetu cha Patanisho,Bwana Kevin alifunguka wazi na kusema kuwa anaomba apatanishwe na shemeji wake kwani anaona huenda shemeji wake atamsaidia kupatana na mke wake.

Gidi alipompigia shemeji wake Kevin,Bwana Bernard,jamaa huyu hakushika simu na hivyo basi maji yakazidi unga kwani mke wake Kevin alisema kuwa ni lazima mume wake azungumze na ndugu zake ndiposa aweze kurudi nyumbani.

Zaidi ya hayo,ilimbidi Kevin amuombe msamaha shemeji yake redioni hata kama Bernard hakushika simu.

''Naomba tu anisamehe kwa sababu sisi wote ni binadamu na tunaweza fanya makosa.''Kevin alisema.

Je una maoni yepi ya kumpa Kevin?