Penzi la sumu: Jinsi mwanamke alivyomhadaa na kumuua mume wake wa zamani kinyama

woman
woman
Wakati  Mary Wanjiku  na mume wake  Kelvin Maina walipotengana kila mmoja walitarajia kuendelea na maisha yake .  Lakini mawasiliano walioanza kubadilishana  kupitia jumbe za simu yaliwapa matumaini kwamba huenda wangerudiana na kuendelea na maisha yao .

Bila kujua kilichokuwa kinaendelea ,Kelvin Maina  hakujua mke wake wa zamani alikuwa na njama ya  kumuua .  Mshukiwa alifaulu kumhadaa hadi katika nyumba yake  mtaani Mathare na Kumdunga kisu kifunia mara mbili siku ya jumatatu . Baadaye Mary alikamatwa na maafisa wa DCI  na anazuiliwa kwa siku 14 huku uchunguzi kuhusu mauaji ya mume wake wa zamani yakichunguzwa .  Corporal Christopher Samoei  wa DCI pangani  aliongoza uchunguzi uliopelekea kukamatwa kwa Mary  pamojana kupatikana kwa silaha iliyotumiwa kwa mauaji ya mume wake wa zamani katika nyumba yake .

Mshukiwa alikamatwa katika eneo la Muthaiga-Kosovo Machi tarehe 16  na uchunguzi dhidi yake unaendelea.Samoei  amesema kisu kilichotumiwa kumuua  Kelvin kilipatikana na mabki ya damu na kimepelekwa kwa mwanakemia wa serikali kwa uchunguzi zaidi .

Polisi wamesema wanahitaji kuzichukua simu za mshukiwa na mumewe kwa uchunguzi  wa kubaini jumbe walizokuwa wamebadilishana  kabla ya Kelvin kwenda katika nyumba ya mke wake  wa zamani alikouawa .