Maski hiyo ina uzito wa gramu 60 na iliwachukua wasanifu wa bidhaa siku nane kumtengezea mfanyibiashara Shankar Kurhade, maski hiyo spesheli .
" Ni nyembamba na ina mashimo madogo amdogo yanayokuwezesha kupumua ,sina uhakika iwapo itanilinda dhidi ya virusi lakini nachukua tahadhari nyingine’ amesema Shankar
Anapoondoka kwake kwa shughuli za kila siku mfanyibiashara huyo hupenda kujistiri kwa dhahabu ikiwemo mshipi wake , shanga na mkufu vyote vyenye uzito wa takriban kilo moja .
Kurhade -- amesema alipata wazo la kutengezwa maski ya dhahabu baada ya kuona katika vyombo vya habari mwanamme mmja akivalia iliyotenegezwa kwa fedha .
" Watu wanataka nipige nao selfie’ amesema
India imefanya uvaaji wa maski kuwa jambo la lazima katika maeneo ya umma baada ya visa zaidi ya laki sita kuthibitishwa na watu 18,600 kuaga dunia .