Pesa otas! Kenya na Tanzania zaongoza kwa idadi ya mabilionea

The Central Bank of Kenya has issued new generation banknotes following promulgation of a new Constitution which ushered hope for a Newly Reborn and Prosperous Kenya.
The Central Bank of Kenya has issued new generation banknotes following promulgation of a new Constitution which ushered hope for a Newly Reborn and Prosperous Kenya.

Kenya na Tanzania zinaongoza kwa idadi ya watu matajiri katika jumuiya ya Afrika mashariki kulingana na utafiti.

Kulingana na ripoti ya 2019 kuhusu utajiri barani Afrika iliochapishwa mwezi Septemba na benki ya AfrAsia, Kenya inaongoza ikiwa na mabilionea 356, Ikifuatiwa na Tanzania ambayo ina mabilionea 99.

Uganda ni ya tatu ikiwa na matajiri 67 huku Rwanda ikifunga orodha hiyo na mabilionea 30.

Ripoti hiyo inasema kwamba matajiri hao wana utajiri wa dola bilioni 10 na kwamba Tanzania ina tajiri mmoja wa dola bilioni moja.

Barani Afrika ripoti hiyo inasema kwamba Afrika Kusini inaongoza kwa matajiri ikiwa na mabilionea 2,169, Misri 932 na Nigeria 531.

Hatahivyo ripoti hiyo haitaji hata bilionea mmoja mbali na mali anayomiliki.

Katika miji mikuu, mji wa Nairobi unaongoza ukiwa na utajiri wa dola bilioni 49 mbele ya mji wa Dar es salaam ambao umeorodheshwa wa 11 na una utajiri wa dola bilioni 24.

Mji mkuu wa Uganda Kampala una utajiri wa dola bilioni 16 huku Addis Ababa ikiwa na utajiri wa dola bilioni 14.

Kulingana na ripoti hiyo mabilionea wa Afrika ni asilimia 16 pekee ya idadi ya mabilionea wote duniani, huku Afrika ikiwa na silimia moja pekee ya utajiri wote duniani.

Utajiri unaomilikiwa na bara hilo ni dola trilioni 2.2 kwa jumla ambapo asilimia 42 ya utajiri huo unalimikiwa na watu wenye utajiri wa kiwango cha juu au HNWIs.

Kwa ujumla mtu mwenye mapato ya kiwango cha kadri anayeishi Afrika ana mali inayogharimu dola 1,900.

Ripoti hiyo inasema kwamba kuna matajiri 140,000 wanaoishi barani Afrika kila mmoja wao akiwa na mali yenye thamani ya dola milioni 10.

Vilevile kwa mujibu wa ripoti hiyo kuna takriban mamilionea 6,900 wanaoishi Afrika kila mmoja akiwa na mali yenye thamani ya dola milioni 10 ama zaidi mbali na mabilionea 23 kila mmoja wao akiwa na mali yenye thamani ya dola bilioni moja.

-BBC