Peter Waweru aliandikisha historia siku ya Jumatatu baada ya kuwa mkenya wa kwanza kusimamia kipute kinacho endelea cha ubingwa wa Africa.
Waweru alisimamia mechi kati ya Namibia na mababe wa Afrika, Ivory Coast katika mechi ya mwisho ya kundi D huku akisaidiwa na mkenya mwenzwa, Gilbert Cheruiyot na raia wa Lesotho, Souru Phatsoane.
Wasimamizi 56 (marefa 27 na wasaidizi 29) wakichaguliwa kusimamia michuano hiyo ya mwaka huu nchini Misri na shirika la soka barani Afrika, CAF.
Sio wengi walipata nafasi ya kusherehekea hadhi hii kwani majirani wetu, Uganda na Tanzania hawakupata nafasi katika orodha hiyo, na kwa hilo tunamsherehekea Peter Waweru.
Kati mechi hiyo, Ivory Coast waliwanyuka Namibia mabao manne kwa moja huku gwiji wa Crystal Palace, Wilfried Zaha ambaye anapaniwa kujiunga na Arsenali, akiwa mmoja wa wafungaji.
Ambacho wengi hawajui kumhusu Waweru nikuwa yeye ni Daktari wa falsafa na ni mhadhiri katika chuo kikuu cha Kenyatta cha Kilimo na Teknolojia.
Tangu apate beji ya usimamizi wa mechi na FIFA, Waweru amesimamia katika michuano ya kombe la bingwa bara Afrika la wachezaji wasiozidi miaka 20, nchini Niger, Februari mwaka huu.
Kati mechi hiyo, Ivory Coast waliwanyuka Namibia mabao manne kwa moja huku gwiji wa Crystal Palace, Wilfried Zaha ambaye anapaniwa kujiunga na Arsenali, akiwa mmoja wa wafungaji.
Ambacho wengi hawajui kumhusu Waweru nikuwa yeye ni Daktari wa falsafa na ni mhadhiri katika chuo kikuu cha Kenyatta cha Kilimo na Teknolojia.
Tangu apate beji ya usimamizi wa mechi na FIFA, Waweru amesimamia katika michuano ya kombe la bingwa bara Afrika la wachezaji wasiozidi miaka 20, nchini Niger, Februari mwaka huu.