PHOTO: Baada ya kukosa patanisho ya leo, Gidi afichua mahala alipo

gidi (1)
gidi (1)

Kama kawaida, wana Jambo huuliza maswali mengi kila wanapotambua kuwa mtangazi fulani hayuko studioni wakati wa kipindi chake. Mara kwa mara, moja kati ya Gidi na Ghost huenda likizo na hapo ndipo maswali hutiririka studioni.

Hii leo ikiwa siku ya wapendanao, wengi wangedhani kuwa wawili hao wangekuwa studioni pamoja kuwatakia wapendanao siku njema huku wakipatanisha waliokosana.

Hata hivyo, Ghost ndiye aliyewachiwa jahazi na wengi walitaka kujua aliko mwenzake. Mulee aliwaarifu kuwa Gidi yuko katika mkutano wa wanaume, almaarufu, Men's conference.

Katika kongamano hilo, wanaume wanashauriana jinsi ya kuishi na wake zao na jinsi ya kuepuka shida baina yao pamoja na maswala ya kuinua jamii.

Kupitia mtandao wake, Gidi alichapisha picha akiwa kwenye gari na rafikiye Alipo wakiwa safarini wakielekea nyumbani Kanyamwa ambapo anatarajiwa kuhudhuria kongamano hilo.

https://www.instagram.com/p/B8ilJkuARa-/