Soma hapa:
Willy Paul amesema kuwa mamake hajawahi kukutana na picha hizo kwani yeye yupo nyumbani na hanaga zile za kumfuata katika mitandao ya kijamii. Picha hizi zilikuwa za kufedhehesha ukizingatia kuwa Pozze ni staa wa nyimbo za injili. Wakenya katika mitandao ya kijamii walimchamba kweli kwa kuonekana kuasi na kumkufuru Mungu.
"Mamangu hafuatilii Show Biz zangu. Yeye yupo nyumbani. Anachokifahamu mimi ni kijana mzuri." Staa huyu alisema.
Pata uhondo hapa:
"Nandy ni dadangu mkubwa. Namheshimu sana." alijitetea Pozze.
Mwanasiasa Musalia Mudavadi alikuwa kati ya watu waliotoa maoni yao kumhusu muimbaji huyu na kumuomba ajirudi. Mwanamuziki Alaine pia alitoa kauli yake na kusema kuwa wakenya wasimkosoe kwa ukali ila wafanye hivo kwa mapenzi.