(+Picha) : Konde Boy achapisha picha na mamake, wanafanana sana

Staa wa muziki wa Bongo Fleva nchini Tanzania hatimaye amemwonyesha mamake mzazi.

Harmonize ni kati ya mastaa wanaofanya vizuri Afrika Mashariki na Afrika ya kati.

Ni staa na ambaye ana mchango mkubwa katika juhudi za kuufanya muziki wa Afrika Mashariki kufikia upeo wa juu zaidi.

Soma hadithi nyingine:

Picha yake na mamake inatokea baada ya Harmonize kuwa na utata mwingi katika tasnia ya muziki.

Konde Boy aliitema lebo yake ya WCB na kuanzisha vuguvugu lake kwa jina Konde Gang.

https://www.instagram.com/p/B2mc4aJHX20/

Katika mahojiano, staa huyu aliitetea Konde Gang na kutaja watu walio katika lebo hiyo,

“Sisi tunakuwa kila siku na watu wanatupenda. Jamii inatupenda na inatufuatilia sana. Konde Gang ni still WCB.”

Soma hadithi nyingine:

 “Konde Gang itakuwa na mastaa wa wengine sio mastaa. Nadhani kwa sasa umeona Jose wa Mipango Jabulanti, Choppa,Mnyama Mkali, Budda na Mchachambo .”

“You know Young Money right, you know cash money right. Come on why are you asking?” Alisema Harmonize.

Soma hadithi nyingine:

Kwa usemi huu, staa huyu anasema hana matatizo na WCB.

Harmonize sawa na Diamond Platnumz ni baadhi ya mastaa waliowaimba na kuwaonyosha mama zao.

Tazama picha ya mama Harmonize:

 Kando na kuwa staa huyu aliitema lebo yake, Babake Diamond ana mtazama tofauti kumhusu,

Mzee Abdul anahoji kuwa dalili za Harmonize kuwa ana uwezo wa kufanya na kusimamia fiesta zake nje ya nchi ni ishara kuwa mwana kashakua na kwa hivo kutoka kwake ni kwema kwa maslahi yake.

Anadokeza kuwa labda dogo kapewa ushawishi na marafiki wake ili kufanya uamuzi huo.

”Kwanza Naseeb alimuangaikia sana. Kamtufuta kampa sapoti kubwa kamtoa kimuziki,” Mzee Abdul.

“Harmonize sio mtoto. Ukiona mtu anatoka kashakomaa tayari.