PICHA: Tazama jinsi Eliud Kipchoge alivyopewa mapokezi ya kifalme

Eluid Kipchoge pamoja na kocha wake Patrick Sang hapo jana walipewa mapokezi ya kifalme walipobebwa na ndege la kifahari kutoka jiji la Eldoret.

Ndege hiyo ilipitia katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta ili kuongeza mafuta kabla ya kuelekea Austria ambapo Eliud anatarajiwa kuivunja rekodi yake ya marathon na kukimbia chini ya masaa mawili.

Kulingana na Eliud, lengo lake ni kuthibitisha kuwa binadamu ana uwezo wa kukimbia kilomita 42 chini ya masaa mawili. Iwapo ataweza kufanikiwa, ataingia katika kitabu cha rekodi cha Guiness kama binadamu wa kwanza duniani kufanya vile.

Tazama picha zifuatazo.