Picha:Tazama walimu wakirejea shuleni kwa matayarisho ya wanafunzi kurejea

Walimu kote nchini wamefurika shuleni siku ya jumatatu wakingoja serikali kutangaza tarehe ya kufunguliwa kwa taasisi zote za masomo .

Katika shule ya msingi ya  Kihumbuini , Kangemi,  mwalimu mkuu  Hassan Tala  aliwaongoza walimu wake kurejea shuleni huku akiketi mbali na kila mmoja kutii kanuni za kupambana na covid 19 .

Mwalimu mwingine alikuwa darasani akifuta ubao  na kuyapanga madawati ya wanafunzi ili kuweka umbali wa dawati moja hadi la pili .

Katika shule ya   Moi Avenue Primary  walimu na wazazi walifanya ukaguzi wa vyoo .walimu baadaye walifanya mkutano kupanga ratiba yao  pindi shule zitakapofunguliwa .

Wiki jana baraza la magavana lilitangaza kwamba  shule za chekechea zitafunguliwa mwezi mmoja baada ya  shule nyingine kufunguliwa ili kukadiria matayarisho .

Rais Uhuru Kenyatta  anatarajiwa kulihutubia taifa baadaye jumatatu baada ya kuandaliwa kwa kongamano linalofanywa kwa njia ya mtandao kuhusu Covid 19  na ataratibu mikakati ya kufunua nchi na sekta za uchumi na jinsi hali itakavyokuwa sasa baada ya janga la Covid 19