'Please forgive me,' Mpiga picha wa Diamond amuomba Khaligraph msamaha

Kenya na Tanzania wamekuwa maadui kwa muda si tu katika biashara hata katika sekta ya sanaa. Mpiga picha wa msanii Diamond Lukamba amemuomba rappa wa humu nchini Khaligraph Jones msamaha baada ya kukataa kumtumia picha zake.

Ilianza na cheche za maneno kwenye mitandao ya kijamii Jones akiuliza ziko wapi picha zake ambazo alipigwa na Lukamba.

Baada ya Lukamba kumchezea sasa yupo kwenye magoti akimuomba Jones msamaha kwa yale ambayo alitenda.

Akizungumza na Wasafi Media, Lukamba aliomba msamaha na kusema kuwa alimwambia Jones shida ambayo ilitokea ndiposa akakosa kumtumia picha zake.

"I took Khaligraph a photo with Diamond Platnumz. Later, Khaligraph sent me a DM to send him the photos. But I later DMed him to tell him that it might take time since my SD card had a problem." Alizungumza Lukamba.

Jambo la pili alisema Diamond hakuhusika katika kutotumiwa kwa picha hizo.

"No, its not Diamond that asked me not to send the photo to Khaligraph. Diamond respects him so much,Photographers can agree with me that SD cards can mess you up sometime."

Akizungumzia picha ambayo aliposti mitandaoni alisema kuwa hakuwa na ubaya wowote,

"I didn´t think that he would take it the wrong way. I ask for his forgiveness if he feels like I humiliated him. I respect him and I didn´t want to disrespect him. I have seen that Kenyan fans are angry about the issue and I ask that you forgive me." Alieleza.

Wacha tungoje na tuone vile Khaligraph atasema kuhusua jambo hilo.