Polisi wamkamata mshukiwa wizi wa watoto, Bungoma

NA BRIAN OJAMA

Maafisa wa polsi wa kituo cha Webuye wanamzuilia mwanamke mmoja wa miaka 22 raia wa Uganda kuhusiana na njama ya kuiba mtoto katika hospitlali ya kimisheni ya Lugulu eneo bunge la Webuye Magharibi kaunti ya Bungoma usiku wa kuamkia leo.

Josephine Nafuna ambaye ameolewa nchini kenya eneo la Kamukuywa eneo bunge la kimilili alikuwa amefikishwa katika hospitali hiyo kujifungua licha ya kutokuwa mja mzito.

Msimamizi wa hospitali ya Lugulu Jackson Fuko amesema kwamba wauguzi walipomchunguza mama huyo walimpata na viraka tumboni.

Alidai kuwa na mimba na kisha ikatoka na kwamba alijifanya kuwa na mimba kwa hofu ya kuachwa na bwanake. Alisema kwamba alikuwa tayari amepoteza mimba mara nne hapo awali.

Wachezaji wanaolipwa mshahara mnono kutoka bara la Afrika

OCPD wa Bungoma Mashariki Valerian Obore amesema kwamba maafisa wa polisi wameanzisha uncunguzi wa kina kuhusu kisa hicho.