Polisi wanachunguza mauaji ya mwalimu wa shule ya upili ya Ngeria, Eldoret

Polisi mjini Eldoret wanachunguza mauaji ya mwalimu wa shule ya upili ya Ngeria iliyoko Eldoret baada ya mwili wake kupatikana umetupwa katika shamba la mahindi, kilomita chache kutoka shule hiyo.

Mkuu wa polisi wa Kapsaret, Francis Warui alisema kuwa mwalimu huyo, Gloria Sangwatei mwenye umri wa miaka 27 alitoweka kutoka nyumbani kwake siku ya Jumapili, kabla ya mwili wake kupatikana katika shamba hilo la mahindi.

Warui alisema kuwa kamba inayokisiwa kutumiwa kumnyonga marehemu ilipatikana karibu na mwili wake.