Polisi wawasili Ruaka Guango Estate alikoishi mshukiwa wa kigaidi

Baada ya uvamizi wa kigaidi katika eneo la Riverside, polisi waliwasili jumatano asubuhi katika eneo la Guango Mali Ruaka, baada ya kusemekana gari lililo tumika katika utekelezaji wa ugaidi huo kuonekana mara kwa mara katika eneo hilo, na mmoja wa magaidi kuhishi jumba nambari E9 Guango Mali.

Mapema rais Uhuru Kenyatta akihutubia taifa jumatano asubuhi alisema kuwa operesheni ilikwisha saa 9:30 asubuhi, na watu 14 kufariki uvamizi huo wa kigaidi.