"Niliweza kupatana na rafiki yangu Rais Maghufuli asubuhi," Raila alisema.
Raila ambaye ni (AU envoy for infrastructure) aliweza kuudhuria mchezo wa mwisho wa sportpesa huko Dar es salaam jumapili ambapo Kariobangi Sharks waliichapa timu ya bandari 1-0 kwa kujiinua kidogo.
Hapo awali Raila aliweza kupeana mfano na rais wa Tanzania John Maghufuli, ambaye alisema aliweza kufanya jitihadakubwa katika kutokomeza ufisadi, kando na nchi ya Kenya.
Ambayo ilichukua hatua kali.
Raila alivunja kimya chake baada ya kuonekana na mashaka ya hali yake ya kiafya katika uwanja wa Dar es salaam, wakati wa kuzawadiwa kwa timu ya sharks.
Jambo lililoleta mjadala katika mitandao ya kijamii. Lakini baada ya masaa machache Raila alisema kuwa yuko salama katika mtandao wake wa kijamii wa twitter.
"Wapendwa wananchi wa kenya na marafiki,niko salama na afya yangu ni nzuri,asanteni kwa kujali," Raila aliongea.