Raila akutana na Maghufuli kuhusu kulinganisha masuala ya ndani

raila odinga
raila odinga
Kinara wa ODM aliweza kukutana na rais wa Tanzania John Pombe Maghufuli katika nchi ya Tanzania. Kupitia mtandao wa kijamii wa twitter Raila alisema walieza kujadili kulinganisha masuala ya ndani.

"Niliweza kupatana na rafiki yangu Rais  Maghufuli asubuhi," Raila alisema.

Raila ambaye ni (AU envoy for infrastructure) aliweza kuudhuria mchezo wa mwisho wa sportpesa huko Dar es salaam jumapili ambapo Kariobangi Sharks waliichapa timu ya bandari 1-0 kwa kujiinua kidogo.

Hapo awali Raila aliweza kupeana mfano na rais wa Tanzania John Maghufuli, ambaye alisema aliweza kufanya jitihadakubwa katika kutokomeza ufisadi, kando na nchi ya Kenya.

Ambayo ilichukua hatua kali.

Raila alivunja kimya chake baada ya kuonekana na mashaka ya hali yake ya kiafya katika uwanja wa Dar es salaam, wakati wa kuzawadiwa kwa timu ya sharks.

Jambo lililoleta mjadala katika mitandao ya kijamii. Lakini baada ya masaa machache  Raila alisema kuwa yuko salama katika mtandao wake wa kijamii wa twitter.

"Wapendwa wananchi wa kenya na marafiki,niko salama na afya yangu ni nzuri,asanteni kwa kujali," Raila aliongea.