Kiongozi wa ODM Raila Odinga amemtemebelea gavana wa Bomet Joyce Laboso hospitali huko London Uingereza .Odinga aliandamana na balozi wa Kenya nchini Uingereza Manoah Esipisu .
Wawili hao walimtakia Laboso afueni ya haraka wakati wa ziara hiyo .Haijafahamika Laboso anaugua nini lakini amechukua likizo ya matibabu kutoka shughuli zake kama gavana .
Kirui amepepezea chini ripoti kwamba gavana Laboso hajakuwa akitekeleza majukumu yake kwa ajili ya maradhi akisema kwamba amekuwa Nairobi akiendelea na kazi zake .
“ Amekuwa kazini wakati wote huo na hayo ndio tuayoweza kusema .. chochote zaidi ya hapo sasa ni mambo ya kibinafasi ambayo hatuzwezi kufichua’.