Kiongozi wa ODM Raika Odinga amesema ripoti ya BBI Iko tayari kutolewa huku akilalamika kwamba kuna watu wanaopanga kuipinga ripoti hiyo . Odinga amesema wanaoipinga ripoti hiyo ni walionufaika na ufisadi na ukiukaji wa sheria .
Katika kinachoonekana kama kumlenga naibu wa rais William Ruto ,Odinga amesema wanaopinga ripoti hiyo wameanza kuwatia wakenya woga na kuwahonga wakenya kutumia pesa kando na kuchochea vita miongoni mwa wananchi .
Amesema wakenya wanafaa kuwakomesha watu hao dhidi ya kuzuia ustawi wa nchi .
Akionekana kuashirikia uwezekano wa kampeini kali kabla ya kura ya maoni kuhusu mapendekezo katika ripoti hiyo Odinga amesema miezi kadhaa ijayo itakuwa makabiliano kati ya walionufaika na ufisadi na wanaotaka kuleta mageuzi nchini kama vile kuleta nafasi za ajira na kuboresha uchumi wa taifa .Amesema lazima lazima wanaopigania maslahi ya Kenya wavishinde vita hivyo.